Dashboard Builder for Access 2.0 Antivirus Report

Sunday, December 5, 2010

KUWA MUWAZI MOJA KWA MOJA BADO NI SERA NZURI
 Tabia na utamaduni   ni vitu  vinyoweza kumjulisha mtu mmoja kwa wengine kwamba yeye ni nani ,mathalani yeye mambo  haya hayapendi na mambo haya anayapenda,lengo la watu wengi  ni kuwa na amani ya moyo,je ulishawahi jiuliza siku unawezaje kuipata amani wakati wewe haueleweki kama upo kwa  upande gani?ili watu waajue jinsi gani ya kuishi nawe inabidi uwNo table of figures entries found.e  wazi ilibaadae  isije kuja matatizo baadae,mara nyingi  sera ya mtu kuwa straight yaani kukiri moja kwa moja kama  ni nyeusi au nyeupe imekuwa ni shida sana  hapa kwetu Africa na inachukua muda sana watu kuifanyia kazi, hii mara nyingi inatokana na hofu ya kuogopa wanadamu wengine alisema  Beatrice  Nyamburua  kutoka  Nairobi ,utakuta mtu mnapanga naye  maagano ya jambo Fulani badala ya yeye kukataa moja kwa moja ananyamaza kimya halafu mwisho wa siku anakuja  kukuambia kuwa jambo  hilo  haliwezekani hii kweli inauma sana  pia kisaikolojia  ina muathiri Yule unaye  mgeuka,pia  katika Nyanja ya dini kwa wale waamini ni dhambi kumpotezea mtu muda wake kwa  uzembe  wako wa kushindwa kujua kuwa  muwazi moja kwa moja ndoo jawabu  ya jambo ulilofanya.Nilikuwa ofisi moja pale Kenya nafanya kazi ,msaidi wa bosi wa kampuni yetu alikuwa anashauri bosi mambo mbalimbali  kutokana na ofu ya kuogopa akimshauri bosi wake kinyume na bosi wake anavyofikir bosi angemropokea  na hata kumfukuza kazi hivyo anajifanya kuwa yupo mstari wa mbele kumsapoti bosi wake kwa mambo yote mabaya  na mazuri badala ya kutoa  ushauri unaofaa na kuishia kumpotosha kisa anahofia akisema itakavyo atapoteza ajira yake,alafu ikitokea watu wakaanza kumpa changamoto bosi wake ghafla akamgeuka bosi anajifanya kumponda bosi wake  na kumchafulia jina lake kuwa bosi wake ni mbishi,anangania mawazo yake tu  mara bosi   vile wakati wa vikao vyote yeye alikuwa anitikia ndio siku mambo yapoanza kwenda kombo  yeye anaanza kugeuka bosi wake si uungwana kabisa na uzandiki wa hali ya juu maaana haiwezekani make vikao  na katika mchakato wote mpo pamoja na   ulikuwa kimya na kukubaliana sawa mwishoe unakuja kumkana.Nimekuwa nikifuatilia  chimbuko la jambo hili hapa kwetu afrika nah ii kweli naamini inatokana na kutokuwa huru kwa watu na kuwa na hofu juu ya maisha yaani kwa lugha nyepesi  ni kuwa watumwa  wa wanadamu wezeko,japokuwa  kuna sababu nyingine  ambayo ni muhimu na ndoo chimbuko,kuwa viongozi wetu wa awali walipanda mbegu hii na  sisi ndoo matunda ya hiyo mbegu iliyopandwa na viongozi wetu wa mwazo,ukisikate taama ukisia hayo kama walipanda mbegu hiyo basin a sisi tupande mbegu nyingine iliyo nzuri kwa taifa la leo na kesho,kuwa muwazi sasa kwa lolote lile,sema ndio au hapana,Ndugu yangu yangu katika hii dunia kama  unataka kuishi kwa furaha jaribu kuwa muwazi moja kwa moja kweli utakuwa na amani na furaha usiogope hamna mtu kashikilia hatma ya maisha yako ni wewe pekeehuwezi kujua ni  kiasi gani  cha maumivu una msababishia Yule unaye muongopea.
 Tujifunze jinsi ya kumaliza   kiini cha tatizo ,tuache kupanda mbegu ya uongo katika familia zetu ,wazazi wetu walituongopea kuwa watoto  wananuliwa hopitali je unaona huu uongo ni wa kuendelea nao kizazi hadi kizazi?ni muda wa kuwa wa kweli sio waongo  huku  twajua kweli ni upi…,je ushawahi  kuhisi siku kama mwezi mmoja ukaishi kwa ukweli  na sio longolongo,alafu mwezi  ukaishi kwa longolongo  na uongo ni upi mwezi ambao unefanikiwa amani ya moyo?ni kazi ndogo tu sisi kuruhu hali ya kubadilika ndani ya nafsi zetu nasi tutakuwa watu wema na wenye amani kubwa.

No comments:

Post a Comment

THIS IS YOUR PLACE TO COMMENT