Dashboard Builder for Access 2.0 Antivirus Report

Wednesday, December 29, 2010

Saikolojia ya rangi

AINA MBALIMBALI  ZA RANGI YA MAVAZI UNATAKIWA UVAE  MAHALI NA KATKA SHUGHULI TOFAUTI:
Saikolojia ya rangi inachukua nafasi kubwa sana katika maana ya mambo(saikolojia)hapa duniani,rangi inachukua nafasi ya kukutabiria wewe nini unataka kiwe ili ufanikiwe au la,haijalishi ka kama wewe umepangalia rangi au hukupangalia(imetoke kwa kutokujua)maumbile ya dunia yapo kukupatia kile ulichoomba(request)na sio vingine kwa lugha rahisi dunia ina kanuni na inabidi uwe ndani ya hizo kanuni ili ufanikiwe,dunia inakupatia mafanikio  au la,nimeshuhudia mara nyingi watu wengi wanashindwa kufanikiwa katika mambo mbalimbali kwa kuwa nje ya kanuni  na ndoo hii sababu ya kuandika makala hili,dunia ina rangi kuu zifuatazo nyeupe,nyekundu,bluu,njano,green,kutokea hapa rangi nzote nyingine zinatoke hapa kwa mchanyiko wa hizo hapo rangi mfano pink,majivu nakadhalika,mara nyingi inashauriwa kuvaa rangi hizo kuu maana zinatoka ujumbe kamili,kila rangi ina maana kubwa kwenye haya maumbile ya dunia,maumbile ya dunia yanafuata kanuni na yatakupatiakile unakihitaji kulingana na lugha yako.Zifuatazo ni aina za rangi na matumizi yake mahala tofauti na shughuli tofauti,
1.Nyekundu,ni rangi  inayotumika katika kutoa amri(order)au ni ya kiutawala zaidi huwa inaamanisha amri  na lazima jambo Fulani lifanyike ,huvaliwa  na mtu mweye cheo kikubwa zaidi wengine kuwaamurisha wenzake mfano maofisini bosi anapotaka anapotaka jambo au kazi Fulani imalizike kwa muda Fulani siku hiyo huvalia tai yake ya nyekundu na katika kikao utaona jinsi anavyo toa amri watu wanatii na kuogopa,Pia maraisi wa nchi hutumia nyekundu pale wanapoenda kutoa amri au kushinikiza jambo Fulani hii inaweza kwa viongozi wenzake mfano mawaziri,hata wananchi nakweli utaona utekelezaji wa jambo hilo kiurahisi,Nyekundu pia hutumika katika mabadilishano ya kibiashara(negotiation)mfano mwaka huu Barack Obama na  raisi wa Urusi Drimitry Medved walipokuwa pale marekani kufanya maongezi ya kibiasha kati ya nchi zao  Obama alivaa tai nyekundu (alikuwa na sauti kubwa maana yake) na raisi  wa Urusi alivaa blue (aonewe huruma)hii ilikuwa mawasiliano tosha tuu na hawakuvaa kibahati ilikuwa impangiliwa hivyo.
2.Bluu(blue),hii ni rangi ya ulizi(protection)hii ni rangi muhimu sana yaw ewe uonewe huruma na watu wengine,mathalani hutumiwa kwenda kuomba kazi kwa kampuni mbalimbali ni vema ukavaa tai ya blue kipindi cha interview wale wanaokufanyia usahili hata kama utakuwa unaukosefu wa jambo Fulani lazima wakuonee huruma na kuweza wewe kupita,Blue pia huvaliwa kipindi cha ujenzi na mafundi ndoo maana overall la kwanza kabisa lilikuwa la rangi ya blue ikiwa na maana ya ulizi(protection).Blue pia hutumika kipindi cha wewe kusafiri kwenda sehemu mbalimbali unasafiri  vaa blue kuanzia nguo ya ndani   hapa utakuwa una ulizi kamili.Katika majadiliano ya biashara au mengine kama wewe huna nguvu(sauti katika hayo)vaa blue huruma itawajia wale unaofanya nao mazungumzo na hivyo kuto nyonywa

3.Njano,hii ni rangi ya umakini hii hutumika kama unataka watu waweke umakini kukusikiliza wewe na kuelewa kile unachokisema  sana sana kwenye hotuba,mahubiri,semina,mikutano nk ni rangi husika kuvuta umakini kutoka kwa watu,vile vile njano hutumika katika kusoma,au kuwa busy juu jambo Fulani hivyo kuonyeshea wengine kuwa wewe upo katika hali ya kutotaka usumbufu wa aina yeyote ile na hivyo  kukuacha na umakini wako,mfano ukiwa unasoma unashauriwa kama hutaki usumbufu kutoka kwa wengine vaa njao utaona jinsi utakavo kuwa huru.
4.Green,ni rangi muhimu sana inayomaanisha kuzidi kukua na kuimarika mfano kampuni au jambo Fulani.Green ni rangi ya mimea  na mimea imeenea kote ulimwenguni hivyo green katika maumbile ya dunia inamaana ya kusambaa au kukua na kuimarika mfano pale kampuni inapotaka  kukua kwa kasi na kusonga mbele kwa kasi utakuta  wafanyakazi wamevalia t-shirt green hapa kuna maana kubwa sana kwa maumbile ya dunia,Kenya ilipopitisha na kuanza kuyatekeleza maono(vision)2030 iliweka rangi ya green  hii ilikuwa na maana kubwa sana katika maumbile ya dunia kuwa Kenya inazidi kukua na kusonga mbelembele  hii rangi Kenya haikuweka kibahati ni plan ya wao kuendelea.


5.Nyeupe,ni uwepo wa rangi zote hutokana,nyeupe hutumika katika maeneo ya ibada,sherehe za amani na furaha,nini nyeupe ina maani kwa maumbile ya dunia?nyeupe inaonyesha usafi wa mtu rohoni,utayari wa kusaidia watu wengine,amani ya mtu kwa watu,yaani mambo yapo
salama,pendelea kuvaa nyeupe wakati wa ibada za kufunga,meditation,sherehe za kusaidiaa watu wenye shida,sherehe  na matukioyanayo maanisha amani
Wengi nazani mtajiuliza je nyeusi je?nyeusi ni kutokuwepo kw rangi yeyote,hivyo nyeusi si rangi,katika maumbile ya dunia huja yaambia jambololote lile hivyo lolote lile linaweza kukuadhiri wewe kwa sababu haupo kwa rangi yeyote,
Mchanyiko wa hizo rangi hapo juu ndoo tuna pata rangi nyingine chungu nzima mfano pink hutumika wakatik machombezo na mpenzi wako,ukiwa upo ndani pink ni rangi ya mahaba na ni nzuri wapenzi wakiivalia wakiwa katika stori za mahaba.
Matuki na aina za rangi
Interview-blue
Kusafiri-blue
Kutoa amri-nyekundu
Msibani-blue
Kuhutubia/kufundisha-njano
Kukua na kuimarika-green
Kusaidia jamii-nyeupe
Kutaka watu wakukubali-blue
Tumia rangi sasa ikupatie  ikupatie mahitaji yako,lolote tukio utakalo lifanya litende kwa umakini na uhakika sio tu kufanya mambo kwa kubahatisha na mwishoe kuwa mtu wa ajabu
Ukitaka kuendele mafanikio yapo mikononi mwako amua leo.

Thursday, December 23, 2010



                                        MAFANIKIO HAYAJI PALE ULIPO UNAFUATA:
Mwenda  buresi kama mkaa bure,huwa anaogeza maarifa na kujifuza zaidi mithali ya Kiswahili inamaana kubwa sana ,ni ndoto au wishes za kila mtu kuwa na mafanikio makubwa sana duniani,lakini kuna tofauti na watu wenye  malengo yaliondikwa kwa karatasi na kuanza kuyatekeleza hawa hugeuza wachotaka kuwa  kuwa kweli  nakuruhusu  mabadiliko ya mafanikio  katika maisha yao,dunia ilivyo sasa ni utandawazi ,taarifa ndio ufunguo wa maisha na sio elimu tena kama ilivyokuwa awali kama huna taarifa juu jambo Fulani basi sahau kuhusu hilo jambo kulifanikisha,mathalani  nilikuwa Kenya nilikutana na Wagerman wengi sana lakini kilichonifurahisha wengi wao walikuwa ni wanafunzi wa political science,sababu tu pekee walioniambia kwa nini walienda Kenya ilikuwa  ni kutaka kuwa bora katika soko laajira linalowangoje baadaye,katika hali za kawaida  mara nyingi huwa tunasikia matangazo ya ajira za kimatifa lakini ni wangapi ndugu zetu huwa wanafikia viwango vyakuchaguliwa  achana na vile vya kisiasa ambavyo huwa tu mtu huchagua kwa kuwa alijifunga na ahadi zake tuje hizi unaenda kushindana na wenzako mnapewa nafasi sawa wengi huishia sakafuni sababu tu  ya kile wanachokijua bado ni kidogo,ndugu zetu huwa  mara nyingi wanaoshiriki  mashindano ya kimataifa  mfano zain Africa challenge huwa hurudi ni kwa sababu tu wamekosa nini jiulize?mara nyingi ndugu zetu huishia kusoma na kukariri sana na kusahau kuwa mbona wapinzani wao hawatumii njia wanayotumia  huwa watu wan chi zinazochukuwa huwa  wanafunzi wao  huwa yale maswali wanayoulizwa huwa ni maisha yao  ya kila siku na sio kama kuanza kuingia mitandaoni kusoma na kwa kukesha .
   Ndugu yangu kwa mantiki hii dunia  imekuwa utandawazi,watu sasa wanapigania kuijua mitaa ya hiki kijiji ili wajue ni jinsi gani wataweza kusurvive katika hiki kijiji,kama wewe unafahamu tu mkoani kwao tu,je jiulize leo utaweza kushindana kibiashara,soko la ajira na mtu aliyetembea nchi zaid kumi?utapotea na kumezwa tu kwa maana huyu  aliyetembea ,mitaa mingi zaidi anaijua njia vema,kwa namna yeyote ile ufuhamu utatofautiana,huyu atakuwa na kadunia kake na Yule atakuwa na dunia yake ,ni muda sasa wa kuchukua hatua ndugu yangu ,utafiti unaonyesha watu  ambao wameishi katika makazi yao toka wazaliwe na kuishi hapo hapo mpaka uzeeni kwao uwelewa wao wa mambo  unakuwa mdogo na wakubabaisha,na pia mimi nasema kuwa mafanikio yao ni madogo  huishia katka janga la umasikini wa kujitakia maana ndio umasikini afrika upo,katika uchunguzi wangu niliufanya katika kulinganisha watu wa aina mbili mmoja kaishi ulaya na mwingine kaishi Tanzania  umri wao wote niligundua tofauti ya uelewa ipo kubwa kati ya pande mbili,hivyo katika  watu wanaoishi kijiji kimmoja maisha yao yote hapa Tanzania   na wale waliohama kijiji mara kwa mara ulewa wao na mafanikio yao huwa ni tofauti ndugu yangu tupo katika dunia mambayo ni lazima  ili ufanikiweuweze kujua wezako wako wapi ili uweze wewe kupiga hatua,hii  ndoo jibu tosha la wewe kuweza kufunguka maishani mwako exposure ni muhimu,katika nchi yetu inasemekana kuwa asilimi kubwa  ya waliopata exposure nje ya nchi ndoo waiendesha  nchi hii    ndugu yangu napenda kukuambia kuwa kuwa mafanikio hayaji tu pale ulipo bali wewe unayafuata yalipo,acha kuku mtaani muda wote,acha kukuaa nyumbani masaa yote toka nje uyafuate mafanikio jichangane katika social event,music concerts,national events na kadhalika utapata kufunguka hakika,acha leo kuwa na maisha ya pembe tatu,yaani kuwa na ratiba fixed,mfano ukitoka kazini au shuleni unaelekea nyumbani na sehemu ya mwisho kuhudhuria ni maeneo ya dini,haya sio maisha ni kama upo kwenye gerza lako wewe mwenyewe,jifungue sasa upate kufunguka na kufanikiwa,mathalani kama wewe ni majsiriamali anza sas kuhuudhuria international event/exhibition,penda kujuana na wengi pasipo kikomo,kuwa tayari ya kulipia gharama ya mafanikio yako an uweze kupata funguo ya mafanikio yako.

Memory zetu inawezekana kuwa fanisi


                         JINSI YA KUWA NA KUMBUKUMBU VIZURI :
Mwaka  2009 nilikuwa mzumbe university nilikuwa katika somo la IT(Information technology)nikapata wazo kama kweli vichwa vetu vingekuwa ni komputa kirahisi tu ningewashauri watu waongeze chip za komputa  ili kuongeza kiwango cha kutunza kumbukumbu vichwani(ubongoni) mwao,lakini ubongo wa mwanadamu ni mashine ambayo  ipo na mambo chungu nzima kuliko kifaa/mashine yeyote ile ya kisasa,hivyo basi kama mtu anataka kuboresha kumbukumbu kichwani anahitaji juhudi Fulani hivi,chukulia mfano ni kama mtu anayekwenda  kufanya mazoezi ya kunyanyua  vitu vizito kadri anavyo zidisha  na kuweka juhudi ndoo  mishipa na misuli yake inavyozidi kutanuka hivyo hivyo katika kuboresha utunzaji wa kumbukumbu inafanya kazi wa kukumbuka unaongezeka kadri unavyofanya mazoezi ya kutunza vizuri kumbukumbu.Kuna aina kadhaa ya vitu vya kutunzia kumbukumbu mfano twasira ya picha,sentensi,mizaha,njia za loc, nk.Zifuatazo ni  namna  mbalimbali za kuboresha utunzaji wa kumbukumbu vizuri:
 1.Mazoezi ya mara kwa mara,husaidia kuongeza oxygen kwenye ubongo ,hivyo kupunguza majanga ambayo  hupeleke kutoke kupoteza kumbukumbu mfano wa magonjwa  kama kisukari na  cardiovascular.
2.Jaribu kuthibiti msongo wa mawazo(stress),Msongo hupelekea kuharibu hippocampus zetu,pia msongo wa  mawazo hupelekea kuwa ni vigumu mtu kulifuatilia jambokwa umakini,hapa nashauri kufanya meditation inasaidia kutatua tatizo.
3.Kuwa na tabia ya kulala vema,kulala ni muhimu sana katika kuimarisha utunzaji mzuri wa kumbukumbu ,ulalaji wa chini ya masaa saba unasababisha mtu kushindwa kufuatilia jambo kwa umakini pia ulalaji wa kupitiliza masaa nane  mfano mtu kulala masaa tisa husababisha matatizo.
4.Acha tabia ya kuvuta sigara,uvutaji wa sigara huzidisha matatizo katika viungo vyetu  ambapo hupelekea mtu kupata magojwa ya mshituko(stroke) na pia kuziba mishipa inayokwenda kupeleka oxygen kwenye ubongo.
5.Kula vizuri na sahihi,tafiti  zinaonyesha kuwa kuna aina za vyakula vinavyo saidia kuboresha utunzaji wa kumbukumbu ,mfano matunda,mboga za majani,wanga, nk,vitamin B san asana B6 na B12 mfano spinachi,melon,maharagwe ya soya,matunda ya citrus nk,pia vitamin C and E mfano nyanya za nyekundu,karanga,mbegu,samaki wa maji baridi,na mafuta ya walnut
6.Husiasha viungo vingi ikiwezekana,hata kama wewe unajifunza kwa kutizama  soma unachojifunza kwa sauti  kile unachotaka kukumbuka,hata kama unaweza kukiwekea katika melodi ya nyimbo ili ukiimbe fanya hivyo,hapo  utakuwa umehusisha viungo kama macho,mdomo,mkono nah ii inasaidia sana  mambo yakiwa mengi hujui la kufanya nk.
7.Pangilia taarifa zako,jaribu kuandika taarifa zako kwenye kitabu kwa mpangilio wa tarehe na  taarifa nyingine muhimu.
8.Penda kuwa muelewa  ,achana na tabia ya kukariri anza na  kuweka tabia ya kuelewa jambo na kuliweza kulieleze kwa lugha yako  mwenyewe.
9.Husisha kile ulichokielewa na  kwa kiunganisha na taarifa mpya kwa taarifa ulielewa kabla ili kutengeneza kitu kimoja kikamilifu.
Kulingana na tafiti mbalimbali  wanadamu wengi inasemekana hutumia asilimia ndogo sana  ya ubongo wao hii utokana na uvivu,au kukosekanika kwa maarifia,mfano  katika asilimi mia  mwanadamu wa makamo hutumia asilimia tano tu,hii nyingine hubaki bila kutumika ,anza sasa kuutumia ubongo wako ukuuletee mabadiliko,wewe unauwezo mkubwa sana wa kutunza kumbukumbu na kuweza kuletamabadiliko anza leo.

Monday, December 20, 2010

hakika furaha ya kweli ni haki yako , an ya kila mtu....



JINSI YA KUPATA FURAHA YA KWELI
Mama Teresa anasema peace begin with smile!na je wewe ushawahi kujiuliza siri ya furaha ya
kweli ni nini?Kuna siku ulishawahi kujiuliza furaha siri yakeni kuwa na fedha tu?vipi kuhusu
umaarufu,nafasi katika madaraka ya nchi au kampuni fulani maarufu hapa Tanzania,je hivi vyote na
vingine vingi vyaweza kukupa furaha ya kweli?Lakini mbona ndoa za matajiri kama Donald Trump na
watu maarufu duniani hazidumu au hazina furaha?achana na hilo mbona pia ndoa na familia za watu
masikini wengi pia zimekosa furaha? Hapo hapo kuna matajiri kama Bill Gates na pia watu wenye
kipato kidogo sana kama Mama Teresa wana furaha sana duniani,ndugu yangu dunia imetengenezwa
kwa kanuni na pi mambo ya dunia yote yana kanuni ukiwa nje ya kanuni hizo katu huwezi kunufaika
nazo,siri ya furaha ya kweli ni maarifa ambayo mtu unatakiwa ujifunze na sio mtu anazaliwa
nayo,maarifa yafuatayo ukiyafuata nina uhakika utapata furaha ya kweli:
Penda kujitolea katika kazi za kijamii,kuwa mstari wa mbele katika mambo ya
kijamii,muungwana,kusaidia wana jamii mfano unaweza kwenda hospitalini ukaenda kuwajulia ali
wagonjwa na kuwapa msaada.
Jipende kwanza wewe,usiwe mgumu juu yako,hakuna mtu mkamilifu,Grace Matata anasema
kujipenda inaanzia kwa mimi kisha upendo unasambaa kwa wengine,penda maisha katika hali zake
zote,
Usiupe nafasi ushauri hasi uingie nafsini kwako,tumezungukwa na dunia isiyo na watu
wakamilifu,kuwa mtu muwelewa wakati mwingine tunaofautiana kwa sababu ya mtizamo
tofauti,ukitaka kujiweka katika nafsi ya mtu kutaka kujua kwa nini manasema hivi au vile unaelekea
kuvunja ukuta wako wa chuki,yasikusumbue maoni mabaya ya mtu kamwe.
Penda kuwa rafiki wa kila mtu,kuwa rafiki kwa kila mtu unayekutana naye,kuwa rafiki
haimaanishi kuwa kila unayekutanaye umpeleke kwenu la hasha bali kuonyesha tabia njema mbele ya
wengine,mwandishi mmoja anasema,when you give positive vibes you will attract positive vibes.
.Kuwa wewe mwenyewe,usipende kujilinganisha na wengine,kila mtu yupo tofauti hapa duniani
hakuna aliyefanana na wewe au uliyefanana naye,jisikie vizuri na njema kuwa wewe unakila kitu
ukijumuishana roho nzuri.
Samehe na sahau,mathalani upo ndani ya daladala mtu kakukanya mguu na kukuomba
msamaha samehe,kusamehe sio kazi rahisilakini ukisamehe unapata ghafla amani ya moyo,samehe
kwa manufaa yako kama siyo ya wale.
Fikiri chanya muda wote,prof wangu chuoni Mzumbe, prof mevdshet anasema positive is more
powerful than negative, mara zote ukiongea hasi unonyesha kwa watu nini kimepungua ndani
yako,nguvu ya chanya itakufanya kila ufanyalo ufanikiwe pasipo kipingamizi kitakacho athiri furaha
yako.
Acha kuweka assumption,kumfikiria mwezako vibayo au kumwekea makadirio mabaya
itakuletea maumivu juu yako mambo yatakopakuwa tofauti na unavyohisi,dunia hii ya watu wastaarabu
na wewe ni mmoja wapo watu huwa wanaongea kwa mamlaka fulani yaani kwa ushahidi na sio
minongono na lawama zisizo za kweli.
Usichukilie vitu kibinafsi,mimi huwa nasema ukisha kuwa maarufu yaani unafahamika kwa
zaidi ya watu wawili,hapo tena una share maisha na wengine hivyo angalia unapofanya maamuzi si
kama wewe bali kundi zima unalo-share nalo maisha linufaike na maamuzi hayo
Ndugu yangu asilimia kubwa ya watu duniani masikini na matajiri huwa mara nyingi wanajikuta
wanaishi maisha yasiyo na furaha na kutamani kujiua mara nyingine sababu huwa ni ndogo sana
kukosa maarifa kuwa kutokuwa na furaha ni wao wenyewe walichagua,pia vilevile unapoona mtu an
furaha ujue pia amechagua hayo maisha,chagua sasa furaha ya kweli,kwani mtu mwenye furaha ya
kweli ni mtu mwenye mafanikio makubwa sana hapa duniani.
                                              Tyra moja ya show zake

Thursday, December 16, 2010

TOO MUCH TALKING......listen twice as talk


KUONGEA SANA  INAWEZA KUKUSABABISHIA WEWE UKOSE  FURSA ZA NAFASI NA MAARIFA KUTOKA KWA WENGINE:
Binadamu ameumbwa  na macho mawili,masikio mawili hii ni viungo muhimu sana katika kumpatia mwanadamu taarifa kutoka kwa wengine,mdomo ni mmoja tu kapatiwa na kutufanya sisi  kutoa taarifa kwa wengine,kwa mantiki ya kawaida hii inamaanisha kuwa wewe  unatakiwa kupokea mara mbili  zaidi ya kile unachokitoa kwa wengine,nahii haina ubishi na haijalishi wewe ni nani au unafanya nini hii ndio sheria iliyo toka enzi na enzi kuanzia china ,ulaya,Afrika na kote duniani wengi watoaji taarifa za kutoka kwao kuliko kupoke huishia kuwa wepesi wa mwili,fikra na kukosa kujiamini kwa mambo yao kwa kuwa hawana jipya au jambo wengine hawalifaamu na kuishia kuwa watu wa kawaida sana na kuwanufaisha wenzao kukua,utaweza jiuliza sana kama ndoo hivyo kwa nini mtu kama mwanasiasa au mchungaji au shehe wanawahuburia sana watu wao lakini kila siku bado wapo imara sana ,sheria ipo pale pale hapa sio kama hawapati taarifa kutoka kwa wengine huwa wanapata sana mfano kupitia kusoma biblia,quruani, novel na vitabu vingine,pia,meditation, kuangalia movies,taarifa za habari hivi  vyote ni vyanzo vya kupata taarifa
Katika maisha  ya kila siku nimeshuhudia  vilio mbalimbali kutoka kwa watu wakijilaumu  na kusema wao si chochote hapa duniani na kweli wenzao hawawathamini  na kamavile wametengwa pasipo  maagano rasmi ya kutopokea taarifa muhimu kutoka kwa wengine,lakini ukiangalia chanzo  cha tatitizo linatokana na wao kuongea sana na kusababisha wao kufukuza maarifa kutoka kwa wengine na taarifa nyingine muhimu .Dunia  hii ndugu imeumbwa na kanuni na jinsi ya kuishi inabidi tutumie kanuni kwa yeyote Yule anayeenda kinyume na kanuni hizi  lazima aangalie wapi alipokosea na arudi nyuma ili asahihishe kosa anza sasa kuwa mjanja kataa taarifa zako kila mtu akazijua hata kama ni mkeo,mzazi au ndugu yako shirikiana nao lakini sio kwa kila taarifa uliyokuwa nao namaanisha kuwa na siri au” msiri” ,binadamu aliyekosa usiri anamatitizo Fulani maana hata mungu ni msiri sana ili shetani kwa wale wanaomaamini asimpiku jaribu kupokea  kutoka kwa wengine  zaidi au soma vitabu sasa,
Njia nyingine ya kutokuwa mzungumzaji sana ni kupenda kuyachukulia mazungumzo  yako ni ya kawaida na sio ya ushindani kwa wengine lengo ni kufikia muafaka. Tatu,unapoona mtu anazungumza acha kumkatisha msubirie mpaka atakapo maliza,na hata kama ataongea sana itafika wakati yeye atatambua wewe pia unahitaji kuongea, hakuna mtu mkamilifua jua hilo.
Mara zote huwa nasema huwa tunafukuza ndoto za kufanikiwa pale  tunapochukua muda wetu kuongea sana kwa kupitiliza anzan sasa kutafuta taarifa muhimu kuliko kutoa ovyo ovyo taarifa  soma  sana vitabu humo ndiko kuna taarifa muhimu,udhuria mikutano muhimu,soma magazine mbalimbali kama fobres magazine kweli utafanikiwa mafanikio ni kwa wote maana dunia  ni yangu na wewe na wengine wote.

Sunday, December 12, 2010

TUNAISHI KWA KUTEGEMEANA ACHA VITA
Dunia sasa imegeuka kijiji ,utandawazi ndoo sera inayoendesha ulimwengu ,mikono yake ipo
kila mahali uanpokuwa ukiwa nje ya kanuni za utandawazi itachukua muda wewe kuendelea,soko
huruia ndoo inaangaza dunia zima kuanzia USA,UK,Tanzania mpaka China na kote duniani,kila mtu
anapigania kuwa na mtandao wa marafiki,business partners wengi kwa wingi pasipo kikomo,wengi
wanapigania kujifunza tamaduni za wengine kwa kasi ili waweze kusurvive katika hii dunia maana
ndoo sera inavyosema.Je ulisha wahi kujiuliza siku ukianzisha au vita unayo sasa kupigana au
kutoelewana na wezako huoni ni kizingiti ndugu yangu,kuna watu wengu katika utafiti wangu mdogo
nimegundua wanashindwa kuendelea kwa kuwa ya kuwa na maadui,kuna mwanamziki wa Uganda
Jose chameleon alisema ameamua kumaliza beef yake na Bebe cool kwa kuwa ina msababishia
kukosa deal kubwa za kuimba nje ya nchi na pia ndani ya nchi,hii ilikuwa yu sababu ya kuacha beef na
siyo sababu nyingine.Ndugu yangu dunia ilivyo kutokea kipindi kilichopita ni katika mtizamo wa huyu
kashinda na huyu kashindwa(win loose) na kweli mtizamo huu sio mzuri na ndoo unasababisha vita na
mtafaruku katika jamii na ndoo huu unasababisha vita tokea enzi na enzi hapa duniani lakini mimi na
wezangu baadhi ya waandishi tunasema hapana sasa ni yatosha tuanze kuishi win win sides(pande zote
zote zimesinda)hakuna aliyeshinda,nilibahatika kuangalia mashindano fulani ya mziki baadaya
kutangazwa mshindi ndipo ugomvi kupitia wasanii ukafumuka nikagundua win loose imewaathiri,hata
sasa sera ya dunia ndoo inavyosema hivyo juzi tulikuwa na uchaguzi hapa Tanzania,upande wa
zanzibar baada ya DR Shein kutangazwa mshindi Mpinzani wake Maalim Seif alisema sote
tumeshinda,wewe leo unangania uitwe mshindi yule aitwe kashindwa baada ya hapo kweli utakuwa
na amani kichwani ukifikiria adui wako?Ndugu yangu kila mwandamu anhitaji kuungwa mkono na
kupewa matumaini na mtu mwingine,chukulia wewe ni mfanya biashara unahitaji wateja wa bidhaa
zako huwezi kupata kipato kama huna wateja,je embu jiulize kama una adui wengi huoni kama ni
kizingiti katika kuogeze kipato kwako?tena inakuwa mbaya ukianzisha vita halafu huna jeshi hapa
ndugu yangu ni mbaya sana watu kumaliza kwa kubomoa misingi ya kazi yako na kufika
tamati(mwisho)pasipo kujijua na kuanza kutapatapa,Martin Luther king anasema kama huwezi
kupigana na sisi basi jiunge na sisi.Sasa ni jinsi gani ya kuungwa mkono na wengine haitaji kutumia
nguvu ili watu wakukubali njia rahisi na yenye tija ni kuwajali,kuwaheshimu na kuwathamini watu
haijalishi ni nani,kitaalamu haijalishi ni wapi anatokea Afrika,ulaya au wapi binadamu yeyote anahitaji
kupendwa na anahitaji kuona yeye wa thamani.
Zifuatazo ni njia unazoweza kutumia kuonyesha una wathamin binadamu wengine:
1.Penda kuwasalimia watu kwa vifupi vya hadhi ya majina yao mfano Mr,Mrs,Miss,Dr,Prof,Sir na
kadhalika ,wasalimu kinyenye kevu na kibusara
2.Mara zote tumezungukwa na dunia iliyo na watu wasio wakamilifu mfano kuna maneno ya
umbea,wivu,uongo sehemu tunamofanya kazi,ishi na kadhalika ndugu yangu kama huwezi kuonge
chochote kizuri au jambo jema kuhusu mtu fulani bora unyamaze kimya.
3.Usujaribu kuwapinga wengine pasipo kuwapa jibu mbadala au njia mbadala iliyo bora ,wapinge
watu katika kuwajenga
4.Mabadiliko yanaanzia kwako na kusambaa kwa wengine, anza sasa kufanya mazoezi ya
kuwathamini wengine anzia kwa mkeo,watoto wako,familia yako,marafiki wako,jirani zako,jamii kwa
ujumla....
5.Wafanye wengine wahisi kuwa wa muhimu sana na hii inakuja kwa kuwaambia kuwa una
wapenda ,unawajali na wao ni watu muhimu sana katika maisha yako nk
Ndugu yangu sisi hapa duniani tupo tofauti wenye mitizamo tofauti na inawezekana sawa ,na wakati
mwingine tupo kwa kazi zinzofanana hata kama ni hivi usichulie ni adui wako bali ni mwezako katika
kukamilisha maono yako.

Sunday, December 5, 2010

NAIROBI.......

KUWA MUWAZI MOJA KWA MOJA BADO NI SERA NZURI
 Tabia na utamaduni   ni vitu  vinyoweza kumjulisha mtu mmoja kwa wengine kwamba yeye ni nani ,mathalani yeye mambo  haya hayapendi na mambo haya anayapenda,lengo la watu wengi  ni kuwa na amani ya moyo,je ulishawahi jiuliza siku unawezaje kuipata amani wakati wewe haueleweki kama upo kwa  upande gani?ili watu waajue jinsi gani ya kuishi nawe inabidi uwNo table of figures entries found.e  wazi ilibaadae  isije kuja matatizo baadae,mara nyingi  sera ya mtu kuwa straight yaani kukiri moja kwa moja kama  ni nyeusi au nyeupe imekuwa ni shida sana  hapa kwetu Africa na inachukua muda sana watu kuifanyia kazi, hii mara nyingi inatokana na hofu ya kuogopa wanadamu wengine alisema  Beatrice  Nyamburua  kutoka  Nairobi ,utakuta mtu mnapanga naye  maagano ya jambo Fulani badala ya yeye kukataa moja kwa moja ananyamaza kimya halafu mwisho wa siku anakuja  kukuambia kuwa jambo  hilo  haliwezekani hii kweli inauma sana  pia kisaikolojia  ina muathiri Yule unaye  mgeuka,pia  katika Nyanja ya dini kwa wale waamini ni dhambi kumpotezea mtu muda wake kwa  uzembe  wako wa kushindwa kujua kuwa  muwazi moja kwa moja ndoo jawabu  ya jambo ulilofanya.Nilikuwa ofisi moja pale Kenya nafanya kazi ,msaidi wa bosi wa kampuni yetu alikuwa anashauri bosi mambo mbalimbali  kutokana na ofu ya kuogopa akimshauri bosi wake kinyume na bosi wake anavyofikir bosi angemropokea  na hata kumfukuza kazi hivyo anajifanya kuwa yupo mstari wa mbele kumsapoti bosi wake kwa mambo yote mabaya  na mazuri badala ya kutoa  ushauri unaofaa na kuishia kumpotosha kisa anahofia akisema itakavyo atapoteza ajira yake,alafu ikitokea watu wakaanza kumpa changamoto bosi wake ghafla akamgeuka bosi anajifanya kumponda bosi wake  na kumchafulia jina lake kuwa bosi wake ni mbishi,anangania mawazo yake tu  mara bosi   vile wakati wa vikao vyote yeye alikuwa anitikia ndio siku mambo yapoanza kwenda kombo  yeye anaanza kugeuka bosi wake si uungwana kabisa na uzandiki wa hali ya juu maaana haiwezekani make vikao  na katika mchakato wote mpo pamoja na   ulikuwa kimya na kukubaliana sawa mwishoe unakuja kumkana.Nimekuwa nikifuatilia  chimbuko la jambo hili hapa kwetu afrika nah ii kweli naamini inatokana na kutokuwa huru kwa watu na kuwa na hofu juu ya maisha yaani kwa lugha nyepesi  ni kuwa watumwa  wa wanadamu wezeko,japokuwa  kuna sababu nyingine  ambayo ni muhimu na ndoo chimbuko,kuwa viongozi wetu wa awali walipanda mbegu hii na  sisi ndoo matunda ya hiyo mbegu iliyopandwa na viongozi wetu wa mwazo,ukisikate taama ukisia hayo kama walipanda mbegu hiyo basin a sisi tupande mbegu nyingine iliyo nzuri kwa taifa la leo na kesho,kuwa muwazi sasa kwa lolote lile,sema ndio au hapana,Ndugu yangu yangu katika hii dunia kama  unataka kuishi kwa furaha jaribu kuwa muwazi moja kwa moja kweli utakuwa na amani na furaha usiogope hamna mtu kashikilia hatma ya maisha yako ni wewe pekeehuwezi kujua ni  kiasi gani  cha maumivu una msababishia Yule unaye muongopea.
 Tujifunze jinsi ya kumaliza   kiini cha tatizo ,tuache kupanda mbegu ya uongo katika familia zetu ,wazazi wetu walituongopea kuwa watoto  wananuliwa hopitali je unaona huu uongo ni wa kuendelea nao kizazi hadi kizazi?ni muda wa kuwa wa kweli sio waongo  huku  twajua kweli ni upi…,je ushawahi  kuhisi siku kama mwezi mmoja ukaishi kwa ukweli  na sio longolongo,alafu mwezi  ukaishi kwa longolongo  na uongo ni upi mwezi ambao unefanikiwa amani ya moyo?ni kazi ndogo tu sisi kuruhu hali ya kubadilika ndani ya nafsi zetu nasi tutakuwa watu wema na wenye amani kubwa.

                   CHUKUA VILIVYO VYAKO HAPA ULIMWENGUNI:
Sayari zipo takribani zaidi ya kumi,japo utafiti bado unaendelea ili kugundua sayari nyingine hapa  ulimwenguni,waweza jiuliza ulimwengu nini?bila shaka kama ni mfuatiliajimzuri wa mambo jibu litakupa ni  muunganiko wa vitu vyote ambavyo ni sayari ambapo ndani yake kuna sayari ya dunia,vitu vingine  vinavyokamilisha neno ulimwengu ni mwezi,nyota,jua  na vingine ambavyo bado kisayansi havijagunduliwa,kila moja  kimoja kinautofauti wake  kutoka kwa kingine,ndani ya sayari ya dunia kuna mengi  kama  milima,mabonde,bahari,wanyama,mimea, binadamu  na viumbe isivyo hai ,lakini cha kushangaza  kila  kitu kipo tofauti na kingine  ukiangalia kwa makini utakuta milima imetofautiana na wanyama,wanyama  wametofautiana na  binadamu yaani kila kimoja kina nafasi yake  na maana yake  yakuwepo hapa kwenye hii sayari ya dunia,katika tafiti na  misemo ya watu mbambali  binadamu  pia wote wametofautiana  maana yake   kila binadamu anajinsi ya tofauti alivyoumbwa kutoka kwa mwingine ,na ndoo maana haijawahi kutokea hata siku moja duniani binadamu wote wakakubaliana  japo kwa sekunde moja dunia nzima na sidhani  kuna siku itatokea,japo kuwa kuna watu mbalimbali wanaoishi ilimradi wamridhishe   au kuna watu wanaoishi kwa kuigana  hii ni katka ulimwengu huu tunaoishi wa” material world” ambapo namba ya material  people inaongezaka  huku namba ya immaterial people inapungua ,lakini turudi hapa,kwanini nasema binadamuwote  tumetofautiana?je kuna siku ulisha wahi  jiuliza natambua mwanadamu mwezangu kwa sura an umbo la mwili wake lilivyo au kwa roho?kama jibu ni kwa roho basi kila mwanadamu ni tofauti  kutoka kwa mwingine,na kila mwanadamu ananafasi sawa kama ilvyo kwa wengine,hakuna mwanadamu aliyemzidi mwingine nikimaanisha kuwa wanadamu wote ni werevu sawa na wajinga sawa mbele za Mungu au hakuna mwanadamu anambania mwenzake asifanikiwe maishani bali ni yeye mwenyewe ana uwezo huo kuamua kufanikiwa au asifanikiwe,hapa wengi hutumia mwili kuamua kufanikiwa wakati wao sio mwili bali wapo katika formless ndugu yangu ili uweze kuwasiliana na wewe inabidi uwe katika umbo lako la formless njia ambazo zinaweza kupeleka katika hali yako ni meditation,sala zaukimya,kutafakari kwa ukimya maeneo mbali na wanadamu,Umbo la mwanadamu ni  vazi tu mwanadamu alipewa ili afurahie maisha ya hapa sayarini achana na nguo wanadamu walizojitengenezeawao wenyewe zinahistoria yake hizi na chimbuko lake.Ndugu yangu ulishawahi jiuliza kuwa sasa kama wanadamu wote ni sawa hasa mbona wengine matajiri na wengine ni masikini?nadhani ni swali linalotekenya kichwa ,ni kweli   napenda kusema hivi dunia iliumbwa kwa principle na  hivyo kama unataka ufanikiwe uwe na furaha ,fedha,kuungwa mkono,kushinda majaribu yote  kuna kanuni  inabidi ufuate ili uweze fanikiwa katika hayo,ndoo maana unaona kati ya matajiri na masikini wa fedha  tofauti ni mambo wanayoyajua na sii kingine ,kanuni za kuwa tajiri zipo wazi,inaaminika wengi masikini wa fedha pia ni masikini wa mawazo ndoo maana wengi wanakata tama kabla hata hawajaweka  nia mioyoni mwao,wengi wanahusishwa na uvivu wa kufikiri kwa angalau siku moja kwa wiki,kumeditate,kusali kwa ukimya   wengi wao wanapenda vitu ambayo tayari vimetaarishwa mathalani kutizama luninga tamthilia Fulani na vipindi kedede  muda wote,kupiga stori san asana kusikiliza kutoka kwa wengine,kucheza tu michezo mbalimbali  muda wote na kadhalika.Haina haja ya wewe sasa kuanza kumuone mwezako wivu kisa kaendelea yule ni Yule na wewe ni wewe hajakushika mashati akuzuie usifanikiwe wala hajachuma mali zako zile ni zake,kila mwanadamu anautajiri mkubwa wa mali  zilizoangukia upande wale ila wanadamu wanashindwa kuzichuma hizo mali .kuwa tajiri ni kanuni haijalishi wewe ni mdhambi au la,bali inajalisha wewe unazifuata kanuni au la ,sio kipimocha  wewe unasali eti sana hii ni  hapana.
Ndugu yangu kama nilivyosema awali wewe upo katika hali ya formless(roho),ukitaka kujua wewe ni nani inabidi uwepo kitika hali yakonjia  ambazo zinaweza kukufikisha hapo ,meditation ni chaguo bora zaidi,sala za ukimya pia ni nzuri,ukishafika katika hali ya  roho sasa anza kujiuliza wewe nini Mungu kaweka nini ndani yako(kipawa) na pia unataka nini katika hii sayari?,jaribu kudadisi kwa makini na taratibu  tizama mfano katika hawa wote  unataka uwe nani,Msanii,Billionea,Mkuu wa nchi,Kiongozi wa dini,Mfanyakazi,Mwanasayansi,Generali wa jeshi,Mtawala katika mamlaka za serikali na organazesheni zake,Msomi, Mwenyekiti mtendaji wa makampuni makubwa,nakadhalika.Hapa ni wakati mgumu  sana kujua wewe ni nani,lakini yakupasa kufuata sauti iliyokuwa inatoka nafsini mwako sio unachoona kwa wengine,tafuta wewe ni nani?taratibu fuata kinachotoka kwako wewe,baada yaw ewe kujitambua sasa anza sasa kukifanyia kazi kile ambacho umekipata hata kam watu watakukatisha tama,njia iliyo bora ni kungangania jambo kama unauhakika nalo haijalishi  ni changamoto zipi unazipata maana wanaokupa changamoto hawana maono wewe ndoo mwenye maono sasa inakuwaje asiyekuwa na maono  na asiyejua jambo kwa nini akuyumbishe?,ndugu yangu ,anza kutafuta ushauri kwa wataalamu wa hilo jambo lakini kuwa makini watu sio usijaribu kutoa wazo lako  wewe taka ushauri binadamu mara nyingi sio waaminifu ,kisha utafanikiwa katika hilo jambo ukiongezeo asilimia kubwa ya nguvu zako,
Siri kuwa duniani kuna mambo mengi sana  chukua yaliyo yako tu na ondoka zako,huu ulimwengu  umejaa mengi makelele  yanachafua hii dunia,wengi wanasema wanavyosema jiulize wewe unasemaje?acha kuiga watu kila mtu ana namna ya kufanikiwa,jiulize kama utaiga ukifika kwa wale wakatishaji tama si utashindwa tu jiamini ndugu yangu.Dunia imejengwa na Mungu kwa misingi ya kanuni na kufanikiwa ni kanuni.Zingatia hili usipende kuropoka ovyo ovyo malengo yako kwa  watu wengi ni waaribu maono ngangania na kile unachokijua ndugu yangu.
                                                                

Saturday, December 4, 2010

MICHAEL....

d                        KUWA MSHINDI KATIKA KULALA VEMA:  
Baada ya kazi na miangaiko mingi ya siku  mara ofisini,nyumbani na sehemu nyingine  mchoko kama huu wote huishia kitandani lakini mara nyingi watu wengi huwa wanalalamika  mara usingizi sipati ,hata muda mwingine wengine hupata usingizi asubuhi  hili tatizo limekuwa kubwa siku hadi siku ndani ya jamii zetu, kitaalamu tatizo la kukosa usingizi huitwa insomnia ,na mara nyingi wengi wanaokumbwa na tatizo hili wamekuwa wakijaribu kutafuta suluhu mbalimbali mathalani wengi  wanajaribu  kutumia madawa ili tu waweze kulitibu tatizo lakini mara zote hii inakuwa suluhu ya muda mfupi tu,siku moja nilikuwa na dada mmoja  alikuwa ananilalamikia kuwa yeye hapati usingizi nahivi sasa yapata miezi sita.kweli ilinigusa sana  na pia aliniambia amejaribu kutumia madawa lakini hayakufua dau kweli hii ni kama kifungo mtu yupo nilimapatia ushauri na baadanya muda aliniambia tatizo limekwisha,katika tafiti mbalimbali mathalani kutoka university of Harvard medical school wanasema kulala ni muhimu sana kwa afya ya mwanadamu muda wakawaida wa mwanadamu kulala kwa usingizi wa afya njema ni masaa manane,utafiti unaonyesha kuwa watu wanaolala kupitiliza masaa nane   mfano wanaolal masaa tisa,kumi nakathalika  huwa wanajitafutia matatizo,inasemekana watu  hawa  kiwango cha waokuishi ni kidogo sana maana ni rahisi kushambuliwa na magonjwa ya moyo mfano heart stroke na mengine  kuliko watu wanaolala masaa ya kawaida nane,miongoni mwa wanaolala masaa tisa kiwango cha kufa ni asilimia286 juu zaidi ya wanaolala masaa saba,vilevile wanaolala masaa chini ya nane mfano matano hukumbwa na matatizo kama kuhisi maumivu kutwa nzima,kutojisikia vema (discomfort) na kwa ujumula  huishia kuthoofika kiafy.
Kuna jinsi yakufanya ili uweze kupata usingi murua na mzuri ,tafiti zinaonyesha mambo yafuatayo yanaweza kukusaidia kuwa na usingizi mzuri kabla ya kwenda kitandani:
 i)Penda fanya mazoezi mepesi kabla ya kwenda kulala,mathalani kunyoosha viungo,puishapu kadhaa
ii)Oga na maji ya vuguvugu  kabla ya kwenda kulala nyakati za usiku.
iii)Sikiliza mziki taratibu na wenye kukuliwaza,ni muhimu sana kununua cd za muziki wa taratibu wakati wa usiku unaiweka na kusikiliza
iv)usipende kwenda kulala wakati huohuo umetoka kula chakula,usipende kuingia kitandani na tumbo lililojaa chakula havita kuletea usingizi
v)Matatizo  yako ya siku nzima usiende nayo kitandani
vi)Kaa katika mawazo mazuri,furaha,amani ya moyo
vii)jiachie mwili wako,akili yako,weka hisia wewe ni mwepesi,weka fikra kuwa usingizi unakuja na jiweke katika mazingira ya kuukubali usingizi

salamu za Kilawe

KUONGEA SANA  INAWEZA KUKUSABABISHIA WEWE UKOSE  FURSA ZA NAFASI NA MAARIFA KUTOKA KWA WENGINE:
Binadamu ameumbwa  na macho mawili,masikio mawili hii ni viungo muhimu sana katika kumpatia mwanadamu taarifa kutoka kwa wengine,mdomo ni mmoja tu kapatiwa na kutufanya sisi  kutoa taarifa kwa wengine,kwa mantiki ya kawaida hii inamaanisha kuwa wewe  unatakiwa kupokea mara mbili  zaidi ya kile unachokitoa kwa wengine,nahii haina ubishi na haijalishi wewe ni nani au unafanya nini hii ndio sheria iliyo toka enzi na enzi kuanzia china ,ulaya,Afrika na kote duniani wengi watoaji taarifa za kutoka kwao kuliko kupoke huishia kuwa wepesi wa mwili,fikra na kukosa kujiamini kwa mambo yao kwa kuwa hawana jipya au jambo wengine hawalifaamu na kuishia kuwa watu wa kawaida sana na kuwanufaisha wenzao kukua,utaweza jiuliza sana kama ndoo hivyo kwa nini mtu kama mwanasiasa au mchungaji au shehe wanawahuburia sana watu wao lakini kila siku bado wapo imara sana ,sheria ipo pale pale hapa sio kama hawapati taarifa kutoka kwa wengine huwa wanapata sana mfano kupitia kusoma biblia,quruani, novel na vitabu vingine,pia,meditation, kuangalia movies,taarifa za habari hivi  vyote ni vyanzo vya kupata taarifa
Katika maisha  ya kila siku nimeshuhudia  vilio mbalimbali kutoka kwa watu wakijilaumu  na kusema wao si chochote hapa duniani na kweli wenzao hawawathamini  na kamavile wametengwa pasipo  maagano rasmi ya kutopokea taarifa muhimu kutoka kwa wengine,lakini ukiangalia chanzo  cha tatitizo linatokana na wao kuongea sana na kusababisha wao kufukuza maarifa kutoka kwa wengine na taarifa nyingine muhimu .Dunia  hii ndugu imeumbwa na kanuni na jinsi ya kuishi inabidi tutumie kanuni kwa yeyote Yule anayeenda kinyume na kanuni hizi  lazima aangalie wapi alipokosea na arudi nyuma ili asahihishe kosa anza sasa kuwa mjanja kataa taarifa zako kila mtu akazijua hata kama ni mkeo,mzazi au ndugu yako shirikiana nao lakini sio kwa kila taarifa uliyokuwa nao namaanisha kuwa na siri au” msiri” ,binadamu aliyekosa usiri anamatitizo Fulani maana hata mungu ni msiri sana ili shetani kwa wale wanaomaamini asimpiku jaribu kupokea  kutokakwa  zaidi au soma vitabu sasa,
Njia nyingine ya kutokuwa mzungumzaji sana ni kupenda kuyachukulia mazungumzo  yako ni ya kawaida na sio ya ushindani kwa wengine lengo ni kufikia muafaka. Tatu,unapoona mtu anazungumza acha kumkatisha msubirie mpaka atakapo maliza,na hata kama ataongea sana itafika wakati yeye atatambua wewe pia unahitaji kuongea, hakuna mtu mkamilifua jua hilo.
Mara zote huwa nasema huwa tunafukuza ndoto za kufanikiwa pale  tunapochukua muda wetu kuongea sana kwa kupitiliza anzan sasa kutafuta taarifa muhimu kuliko kutoa ovyo ovyo taarifa  soma  sana vitabu humo ndiko kuna taarifa muhimu,udhuria mikutano muhimu,soma magazine mbalimbali kama fobres magazine kweli utafanikiwa mafanikio ni kwa wote maana dunia  ni yangu na wewe na wengine wote.

Thursday, December 2, 2010

Kilawe Deogratius mjasiriamali aliyebobea aanziasha new project.........

Baada ya kufanikisha project yake ya  stationary  bab kubwa na lenye kutoa huduma kwa bei nafuu,mjasiriamali na mwandishi wa makala za kuchochea kufanikiwa Tanzania,sasa ameanzisha project yake ya  kuwafundisha watu jinsi ya kutengeneza blogspot kwa bei  ndogo sana  ambayo mtanzania anayeishi chini ya dollar mioja anaweza kuimudumu hii nia idea ambayo Mr Deogratius kilawe analengo la kila Mtanzania kuwa na yake blogspot ,...........,vilevile Mr Deogratius Kilawe  amefungua rasmi  project kabambabe ya kutengeneza website nzuri zenye hadhii ya kimataifa na mishiko kwa watu wote  kwa kampuni za kitanzania  na nje ya kitanzania kwa bei nafuu..... kwa mawasiliano na Deo kilawe unaweza mpata kwa  0717109362 au email:deogratiuskilawe@yahoo.com

How do I put AdSense on my blog (using a classic template)?

kupitia hapa unaweza kutengeneza fedha na google

makala la kwanza.

TUNAISHI KWA KUTEGEMEANA ACHA VITA
Dunia sasa imegeuka kijiji ,utandawazi ndoo sera inayoendesha ulimwengu ,mikono yake ipo
kila mahali uanpokuwa ukiwa nje ya kanuni za utandawazi itachukua muda wewe kuendelea,soko
huruia ndoo inaangaza dunia zima kuanzia USA,UK,Tanzania mpaka China na kote duniani,kila mtu
anapigania kuwa na mtandao wa marafiki,business partners wengi kwa wingi pasipo kikomo,wengi
wanapigania kujifunza tamaduni za wengine kwa kasi ili waweze kusurvive katika hii dunia maana
ndoo sera inavyosema.Je ulisha wahi kujiuliza siku ukianzisha au vita unayo sasa kupigana au
kutoelewana na wezako huoni ni kizingiti ndugu yangu,kuna watu wengu katika utafiti wangu mdogo
nimegundua wanashindwa kuendelea kwa kuwa ya kuwa na maadui,kuna mwanamziki wa Uganda
Jose chameleon alisema ameamua kumaliza beef yake na Bebe cool kwa kuwa ina msababishia
kukosa deal kubwa za kuimba nje ya nchi na pia ndani ya nchi,hii ilikuwa yu sababu ya kuacha beef na
siyo sababu nyingine.Ndugu yangu dunia ilivyo kutokea kipindi kilichopita ni katika mtizamo wa huyu
kashinda na huyu kashindwa(win loose) na kweli mtizamo huu sio mzuri na ndoo unasababisha vita na
mtafaruku katika jamii na ndoo huu unasababisha vita tokea enzi na enzi hapa duniani lakini mimi na
wezangu baadhi ya waandishi tunasema hapana sasa ni yatosha tuanze kuishi win win sides(pande zote
zote zimesinda)hakuna aliyeshinda,nilibahatika kuangalia mashindano fulani ya mziki baadaya
kutangazwa mshindi ndipo ugomvi kupitia wasanii ukafumuka nikagundua win loose imewaathiri,hata
sasa sera ya dunia ndoo inavyosema hivyo juzi tulikuwa na uchaguzi hapa Tanzania,upande wa
zanzibar baada ya DR Shein kutangazwa mshindi Mpinzani wake Maalim Seif alisema sote
tumeshinda,wewe leo unangania uitwe mshindi yule aitwe kashindwa baada ya hapo kweli utakuwa
na amani kichwani ukifikiria adui wako?Ndugu yangu kila mwandamu anhitaji kuungwa mkono na
kupewa matumaini na mtu mwingine,chukulia wewe ni mfanya biashara unahitaji wateja wa bidhaa
zako huwezi kupata kipato kama huna wateja,je embu jiulize kama una adui wengi huoni kama ni
kizingiti katika kuogeze kipato kwako?tena inakuwa mbaya ukianzisha vita halafu huna jeshi hapa
ndugu yangu ni mbaya sana watu kumaliza kwa kubomoa misingi ya kazi yako na kufika
tamati(mwisho)pasipo kujijua na kuanza kutapatapa,Martin Luther king anasema kama huwezi
kupigana na sisi basi jiunge na sisi.Sasa ni jinsi gani ya kuungwa mkono na wengine haitaji kutumia
nguvu ili watu wakukubali njia rahisi na yenye tija ni kuwajali,kuwaheshimu na kuwathamini watu
haijalishi ni nani,kitaalamu haijalishi ni wapi anatokea Afrika,ulaya au wapi binadamu yeyote anahitaji
kupendwa na anahitaji kuona yeye wa thamani.
Zifuatazo ni njia unazoweza kutumia kuonyesha una wathamin binadamu wengine:
1.Penda kuwasalimia watu kwa vifupi vya hadhi ya majina yao mfano Mr,Mrs,Miss,Dr,Prof,Sir na
kadhalika ,wasalimu kinyenye kevu na kibusara
2.Mara zote tumezungukwa na dunia iliyo na watu wasio wakamilifu mfano kuna maneno ya
umbea,wivu,uongo sehemu tunamofanya kazi,ishi na kadhalika ndugu yangu kama huwezi kuonge
chochote kizuri au jambo jema kuhusu mtu fulani bora unyamaze kimya.
3.Usujaribu kuwapinga wengine pasipo kuwapa jibu mbadala au njia mbadala iliyo bora ,wapinge
watu katika kuwajenga
4.Mabadiliko yanaanzia kwako na kusambaa kwa wengine, anza sasa kufanya mazoezi ya
kuwathamini wengine anzia kwa mkeo,watoto wako,familia yako,marafiki wako,jirani zako,jamii kwa
ujumla....
5.Wafanye wengine wahisi kuwa wa muhimu sana na hii inakuja kwa kuwaambia kuwa una
wapenda ,unawajali na wao ni watu muhimu sana katika maisha yako nk
Ndugu yangu sisi hapa duniani tupo tofauti wenye mitizamo tofauti na inawezekana sawa ,na wakati
mwingine tupo kwa kazi zinzofanana hata kama ni hivi usichulie ni adui wako bali ni mwezako katika
kukamilisha maono yako.

DEOGRATIUS ANAWAKARIBISHA WOTE KWA SCIENTIFIC MONEY